3 Machi 2015 - 20:41
Mazungumzo ya amani ya Yemen

Rais wa Yemen leo amependekeza mji mkuu wa Saudi Arabia , Riyadh kama sehemu inayowezekana kufufua mazungumzo yanayosimamiwa na Umoja wa Mataifa pamoja na wanaharakati wa Kishia ambao wamekamata mji mkuu wa Yemen Sanaa.

Rais  wa Yemen  leo  amependekeza  mji  mkuu  wa  Saudi  Arabia , Riyadh  kama  sehemu  inayowezekana  kufufua  mazungumzo yanayosimamiwa  na  Umoja  wa  Mataifa  pamoja  na  wanaharakati  wa Kishia ambao  wamekamata  mji mkuu  wa  Yemen  Sanaa.

Rais Abed Rabbo Mansour Hadi  ametoa  pendekezo  hilo  katika mkutano  na  viongozi  wa  kikabila  kutoka  jimbo  la  kusini  la Abyan, kwa  mujibu  wa  washiriki  wawili  na  msaidizi  wa  rais ambao  wamezungumza  kwa  masharti  ya  kutotajwa  majina kwasababu  hawakuwa  na  ruhusa  ya  kuzungumza  na  vyombo vya  habari.

Wamesema  Hadi  amependekeza  makao  makuu  ya  baraza  la ushirikiano  la  mataifa  sita  ya  Ghuba  kama  sehemu  iwapo wanaharakati  wa  Kihuthi  wataendelea  kupinga  kuyaondoa  mazungumzo hayo  kutoka  Sanaa, ambao  uko  katika  udhibiti  wao  tangu  mwezi Septemba, na  kwenda  ama  Aden  au Taiz  upande  wa   kusini.

Wakati huo huo Mahakama  nchini  Misri  imesitisha  uchaguzi  ujao  nchini  humo  wa bunge, kufuatia  hukumu  iliyotolewa  hivi  karibuni  na  mahakama kuu  ya  katiba ikieleza  sheria  zinazoendesha  uchaguzi  kuwa zinakwenda  kinyume  na  katiba.

Uamuzi  huo  uliotolewa  leo  na  jaji Yahia Dakrouri  wa   mahakama hiyo  ya  utawala  ulitarajiwa   baada  ya  hukumu  iliyotolewa  na mahakama  kuu  wiki  iliyopita.

Kamati  ya  uchaguzi  nchini  humo  baadaye  itapanga  tarehe nyingine  kwa  ajili  ya  uchaguzi  huo.  Kamati  ya  uchaguzi imesema  inafanyia  kazi  kubadilisha  sheria  hiyo.

Uchaguzi  wa  bunge  ulipangwa  awali  kufanyika  kwa  awamu kuanzia  Machi  22, ikiwa awamu  ya  mwisho  katika  kipindi  cha mpito  kufuatia  kuondolewa  mwaka  2013  kwa  rais  Mohammed Mursi  na  jeshi.